MAMBO MATANO YA KUISAIDIA NIGERIA BAADA YA KUSHINDWA KUFUZU AFCON 2017
Kwa mara nyingine Nigeria Super Eagles watakosekana kwenye michuano ya mataifa ya Afrika (African Nations Cup) kwa mara ya pili mfululiz...

http://clemencekarani.blogspot.com/2016/03/mambo-matano-ya-kuisaidia-nigeria-baada.html
Kwa mara nyingine Nigeria Super Eagles watakosekana kwenye michuano
ya mataifa ya Afrika (African Nations Cup) kwa mara ya pili mfululizo
baada ya kukubali kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa Misri kwenye mchezo wa
marudiano na kufanya matokeo ya jumla kuwa 2-1baada ya kucheza michezo
yote miwili.
Kwan nchi yenye wakazi wengi kuliku nchi nyingine za kiafrika, ambayo inatoa wachezaji wengi kwenda nje ya Afrika na imekuwa juu ya soka la Afrika kwa muda mrefu ni jambo la kushangaza kushuhudia Nigeria ikianguka.
Kushindwa kufuzu kwa msimu huu kunaifanya kuyakosa mashindano hayo kwa mara tatu ndani ya miaka minne. Hiyo inaonesha kwamba Nigeria imekuwa kama chambo na kutokana na kiwango wanachokionesha wanatakiwa kuangaliwa kama chambo kwenye soka la Afrika.
Kutambua tatizo ni hatua ya kwanza kuelekea kutauta ufumbuzi, na hapa ndipo Nigeria wanahitaji kuanzia:
Badala ya kurudi nyuma kuangalia kwanini timu ilishindwa kufuzu na kipi kilihitajika kufanywalakini haraka Siasia alitimuliwa kazi. Licha ya kwamba kikosi cha wakati huo kilikuwa kikicheza soka la kuvutia, kilikua pia kinafunga magoli ya kutosha.
Kipindi hiki cha kutafuta nafasi ya kufuzu kwa michuano ijayo, makocha watatu wakiwa na style zao tofauti za ufundishaji na wamewaita wachezaji tofautitofauti kila mmoja kwa kipindi chake. Kila kocha akija na nahodha wake tofauti.
Siasia ameteuliwa kama kocha wa muda, lakini ni wakati sahihi chama cha soka cha Nigeria (NFF) kumpa mkataba wa muda mrefu kuendeleza harakati alizozianza.
Hakuna haja ya kocha mpya kuja tena na kuanza upya kwenye mchakato ambao tayari umeanza kupamba moto.
Tulichokiona kwenye dakika zaidi ya 180 dhidi ya Misri ni wachezaji kucheza soka safi kitimu, kutengeneza nafasi, na kikaonesha kuwa kitakuwa vizuri baada ya muda lakini kinaangushwa na safu ya ulinzi.
Wapewe muda na kwa msaada wa kiufundi wanaoupata kutoka kwa Shaibu Amodu hii ni timu ambayo inaweza ikafika mbali kama wataamua kumpa muda kocha.
Serikali kuingilia shughuli za NFF inaweza ikawa sababu ya kushindwa kufanya kazi zake vizuri. Kusubiri kwa miezi kadhaa kuhusu masuala ya kifedha kukamilishwa hata baada ya bajeti kuwa iko wazi hii inaiathiri timu kwenye maandalizi na mipango yake
Na timu ya kipindi hicho ndiyo iliitambulisha The Super Eagles nje ya mipaka ya Afrika. Wakati huo wachezaji walikuwa na uzalendo na kujiamini na walikuwa wakionekana hivyo katikati ya uwanja.
Nigeria ilimtunza kocha na kumwachia majukumu ya kuijenga tofauti na sasa ambapo wachezaji wamekuwa hawana uhakika kama wataitwa kwenye mechi inayofuata au la.
Ushahidi ambao mtu anaweza kutoa kutokana na michezo hiyo miwili ni kwamba, mfumo ndiyo tatizo. Kwa kipindi kirefu, Ighalo alionekana pekeake akiwa katikati ya mabeki wawili akiwa hana msaada. Kuna wakati alishuka chini na kuchukua mpira akaenda pembeni kisha akampigia pasi Ahmed Musa ambaye alikuwa amesogea katikati ya uwanja lakini alishindwa kuusoma mchezo huo na hakuukimbilia mpira.
Alicheza vizuri baada ya Alex Iwobi kuingia, kinda wa Arsenal mwenye uwezo wa kukimbia na walikuwa wakibadilisha nafasi hali iliyowapa shida mabeki wa Misri
Ni wakati muafaka sasa kwa Siasia kubadilisha mfumo ili uwafit wachezaji anaowatumia. Mashabiki wengi tayari wameanza kumkosoa Ighalo na litakuwa kosa kubwa kwa Siasia kumtema mchezaji huo.
Rashidi Yekini alipoteza nafasi kibao, lakini anajiamini kwasababu anajua kwamba kocha na wachezaji wenzake wanaimani nae. Jambo hili pia Ighalo anahitaji kuwanalo.
Siasia amekuwa na mfumo wa aina nyingine wa kushambulia. Ukifanikiwa ni mfumo unaovutia lakini timu ikishindwa kufunga unakuwa hatari.
Kwan nchi yenye wakazi wengi kuliku nchi nyingine za kiafrika, ambayo inatoa wachezaji wengi kwenda nje ya Afrika na imekuwa juu ya soka la Afrika kwa muda mrefu ni jambo la kushangaza kushuhudia Nigeria ikianguka.
Kushindwa kufuzu kwa msimu huu kunaifanya kuyakosa mashindano hayo kwa mara tatu ndani ya miaka minne. Hiyo inaonesha kwamba Nigeria imekuwa kama chambo na kutokana na kiwango wanachokionesha wanatakiwa kuangaliwa kama chambo kwenye soka la Afrika.
Kutambua tatizo ni hatua ya kwanza kuelekea kutauta ufumbuzi, na hapa ndipo Nigeria wanahitaji kuanzia:
- Kumwacha Samson Siasia aendelee kuwa kocha mkuu
Badala ya kurudi nyuma kuangalia kwanini timu ilishindwa kufuzu na kipi kilihitajika kufanywalakini haraka Siasia alitimuliwa kazi. Licha ya kwamba kikosi cha wakati huo kilikuwa kikicheza soka la kuvutia, kilikua pia kinafunga magoli ya kutosha.
Kipindi hiki cha kutafuta nafasi ya kufuzu kwa michuano ijayo, makocha watatu wakiwa na style zao tofauti za ufundishaji na wamewaita wachezaji tofautitofauti kila mmoja kwa kipindi chake. Kila kocha akija na nahodha wake tofauti.
Siasia ameteuliwa kama kocha wa muda, lakini ni wakati sahihi chama cha soka cha Nigeria (NFF) kumpa mkataba wa muda mrefu kuendeleza harakati alizozianza.
Hakuna haja ya kocha mpya kuja tena na kuanza upya kwenye mchakato ambao tayari umeanza kupamba moto.
Tulichokiona kwenye dakika zaidi ya 180 dhidi ya Misri ni wachezaji kucheza soka safi kitimu, kutengeneza nafasi, na kikaonesha kuwa kitakuwa vizuri baada ya muda lakini kinaangushwa na safu ya ulinzi.
Wapewe muda na kwa msaada wa kiufundi wanaoupata kutoka kwa Shaibu Amodu hii ni timu ambayo inaweza ikafika mbali kama wataamua kumpa muda kocha.
- Soka lazima liwe huru
Serikali kuingilia shughuli za NFF inaweza ikawa sababu ya kushindwa kufanya kazi zake vizuri. Kusubiri kwa miezi kadhaa kuhusu masuala ya kifedha kukamilishwa hata baada ya bajeti kuwa iko wazi hii inaiathiri timu kwenye maandalizi na mipango yake
- Wachezaji lazima waoneshe utayari wao
Na timu ya kipindi hicho ndiyo iliitambulisha The Super Eagles nje ya mipaka ya Afrika. Wakati huo wachezaji walikuwa na uzalendo na kujiamini na walikuwa wakionekana hivyo katikati ya uwanja.
Nigeria ilimtunza kocha na kumwachia majukumu ya kuijenga tofauti na sasa ambapo wachezaji wamekuwa hawana uhakika kama wataitwa kwenye mechi inayofuata au la.
- Kutengeneza mfumo utakaombeba Ighalo
Ushahidi ambao mtu anaweza kutoa kutokana na michezo hiyo miwili ni kwamba, mfumo ndiyo tatizo. Kwa kipindi kirefu, Ighalo alionekana pekeake akiwa katikati ya mabeki wawili akiwa hana msaada. Kuna wakati alishuka chini na kuchukua mpira akaenda pembeni kisha akampigia pasi Ahmed Musa ambaye alikuwa amesogea katikati ya uwanja lakini alishindwa kuusoma mchezo huo na hakuukimbilia mpira.
Alicheza vizuri baada ya Alex Iwobi kuingia, kinda wa Arsenal mwenye uwezo wa kukimbia na walikuwa wakibadilisha nafasi hali iliyowapa shida mabeki wa Misri
Ni wakati muafaka sasa kwa Siasia kubadilisha mfumo ili uwafit wachezaji anaowatumia. Mashabiki wengi tayari wameanza kumkosoa Ighalo na litakuwa kosa kubwa kwa Siasia kumtema mchezaji huo.
Rashidi Yekini alipoteza nafasi kibao, lakini anajiamini kwasababu anajua kwamba kocha na wachezaji wenzake wanaimani nae. Jambo hili pia Ighalo anahitaji kuwanalo.
- Marekebisho kwenye safu ya ulinzi
Siasia amekuwa na mfumo wa aina nyingine wa kushambulia. Ukifanikiwa ni mfumo unaovutia lakini timu ikishindwa kufunga unakuwa hatari.