Didier Drogba kulishtaki gazeti la Dail Mail

Nyota Didier Drogba amesema atachukua hatua ya kiesheria kuhusiana na tuhuma kuwa shirika lake la hisani limetumia chini ya asilimia moja ...

Nyota Didier Drogba amesema atachukua hatua ya kiesheria kuhusiana na tuhuma kuwa shirika lake la hisani limetumia chini ya asilimia moja ya fedha zilizochangishwa kwa ajili ya miradi muhimu
Gazeti maarufu la Uingereza la Daily Mail lilisema kuwa pauni 14,000 tu kati ya pauni milioni 1.7 zilizotolewa na wahisani kwa wakfu wa Didier Drogba zimetumika kuwanufaisha watoto nyumbani kwao Cote d'Ivoire.
Tume ya inayoshughulika na mambo ya hisani nchini Uingereza imesema inachunguza shughuli za wakfu huo ulioanzishwa mwaka wa 2009 na aliyekuwa mchezaji huyo wa Chelsea.
Drogba mwenye umri wa miaka 38, anayechezea klabu ya Montreal Impact ya Ligi Kuu ya Kandanda ya Canada, amekanusha tuhuma hizo katika taarifa yenye maneno mazito ambayo amesema habari hizo za Daily Mail ni za kumchafulia jina.

Related

MICHEZO 6152041115978956954

Post a Comment

emo-but-icon

MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII

KILIMANJARO MOUNTAIN IN TANZANIA

http://www.tanzaniaparks.go.tz/

welcome in Tanzania at Arusha Mount meru

https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=7138641291977024838#editor/target=post;postID=3203923396230239409

https://web.facebook.com/kephasilani?fref=ts

Recent

Comments

item