Kenya yaitaka ICC kuikabidhi faili za washukiwa 3

Mahakama ya ICC Kenya sasa inataka faili za kesi zinazowakabili wakenya watatu wanaotuhumiwa kuingilia ushahidi wa ma...

Mahakama ya ICC
Kenya sasa inataka faili za kesi zinazowakabili wakenya watatu wanaotuhumiwa kuingilia ushahidi wa mashahidi wa ICC kushtakiwa nchini humo.
Mwanasheria mkuu Profesa Githu Muigai amesema kuwa Kenya ina mahakama zilizo na uwezo za kushtaki kesi ndogo kufuatia kuanguka kwa kesi kuu iliowahusisha wakenya sita maarufu kama Ocampo 6.
Mwanasheria huyo pia ameshtumu idara ya mashtaka katika mahakama ya ICC kwa kushindwa kushirikiana na Kenya kuhusu ombi la awali lililowasilishwa kwa aliyekuwa kiongozi wa mashtaka Moreno Ocampo kuikabidhi Kenya faili zote za washukiwa.
Amesema kuwa Kenya ina haki ya kushirikiana na mahakama hiyo au la iwapo ICC itafeli kuikabidhi Kenya faili hizo.
Ameongezea kuwa mpango wa Kenya kujiondoa katika mahakama hiyo utaangaziwa na Umoja wa Afrika AU na kwamba Kenya kama taifa haijaanza harakati za kujiondoa.

Related

HABARI 6253017013455921718

Post a Comment

emo-but-icon

MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII

KILIMANJARO MOUNTAIN IN TANZANIA

http://www.tanzaniaparks.go.tz/

welcome in Tanzania at Arusha Mount meru

https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=7138641291977024838#editor/target=post;postID=3203923396230239409

https://web.facebook.com/kephasilani?fref=ts

Recent

Comments

item