Jamie Vardy ndiye mwanasoka bora wa mwaka

Mshambuliaji wa klabu ya Leicester City Jamie Vardy ametangazwa mshindi wa tuzo ya mwana soka bora wa mwaka na chama cha waandishi wa kand...

Mshambuliaji wa klabu ya Leicester City Jamie Vardy ametangazwa mshindi wa tuzo ya mwana soka bora wa mwaka na chama cha waandishi wa kandanda Uingereza
Mshambuliaji huyo wa Uingereza alipata asilimia 36 ya kura zilizopigwa na wanahabari 290 na kuwapiku wenzake Riyad Mahrez na N'Golo Kante. Vardy mwenye umri wa miaka 29, amefunga mabao 22 ya ligi kuu ya kandanda England.
Pia alivunja rekodi ya kufunga mabao kila mechi katika mechi 11 mfululizo. Leicester City inahitaji pointi mbili pekee ili kushinda Ligi Kuu ya England lakini inaweza pia kutawazwa mabingwa iwapo Tottenham Hotspurs watashindwa kuwalaza Chelsea leo usiku.
Riyad Mahrez raia wa Morocco alishinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka ya PFA, ambayo mshindi hupigiwa kura na wachezaji soka ya kulipwa

Related

MICHEZO 1235218550668942637

Post a Comment

emo-but-icon

MMILIKI WA BLOG HII

MMILIKI WA BLOG HII

KILIMANJARO MOUNTAIN IN TANZANIA

http://www.tanzaniaparks.go.tz/

welcome in Tanzania at Arusha Mount meru

https://www.blogger.com/blogger.g?blogID=7138641291977024838#editor/target=post;postID=3203923396230239409

https://web.facebook.com/kephasilani?fref=ts

Recent

Comments

item