Picha: Maisha ya Beyonce na Jay Z baada ya ‘Lemonade’
Mwezi April, mwaka huu Beyonce alitengeneza vichwa vya habari duniani baada ya kuachia kwa kushtukiza tena album mpya ‘Lemonade’, aliyoelez...
http://clemencekarani.blogspot.com/2016/06/picha-maisha-ya-beyonce-na-jay-z-baada.html
Mwezi April, mwaka huu Beyonce alitengeneza vichwa vya habari duniani
baada ya kuachia kwa kushtukiza tena album mpya ‘Lemonade’, aliyoelezea
kwa mara ya kwanza skendo ya muda mrefu kuhusu matatizo ya ndoa yake na
Jay Z.
Kwenye wimbo wake ‘Sorry’ alizungumzia jinsi ambavyo mume wake [Jay Z] alivyowahi kumsaliti kwa kutembea na wanawake wengine. Mstari ‘You better call Becky with the good hair’ uliopo kwenye wimbo huo uliwaweka kwenye wakati mgumu Rachel Roy na Rita Ora ambao walidaiwa kuchepuka na bosi huyo wa lebo ya Roc Nation.
Skendo hiyo ilitia shaka kuvunjika kwa ndoa yao kutokana na yale aliyoyazungumza Queen Bey ndani ya albamu hiyo. Maisha yamezidi kuendelea huku wawili hao wakionekana kwenye viwanja mbalimbali wakiendelea kula bata pamoja huku ndoa yao ikizidi kuwa na furaha na Jay Z akizidi kutoa mchango mkubwa kwenye ziara ya Beyonce, ‘Formation Tour’.
Ukweli unaonesha kuwa Jay alikubali kuimbwa hivyo na mkewe kwa imani iliyotimia kuwa albamu ya Lemonade ingeingiza mkwanja mrefu na mwisho wa siku wawili hao wataendelea kufurahia mapenzi yao, na mahaba tele. Hiyo inathibitika kama alivyorap Jay Z kwenye mashairi ya remix ya Fat Joe na Remy Ma, “You know you made it when the fact your marriage made it is worth millions. Lemonade is a popular drink and it still is.”
Tazama picha za Queen Bey na Jay Z baada ya Lemonade kutoka na wakifurahia vekesheni ya nguvu
Kwenye wimbo wake ‘Sorry’ alizungumzia jinsi ambavyo mume wake [Jay Z] alivyowahi kumsaliti kwa kutembea na wanawake wengine. Mstari ‘You better call Becky with the good hair’ uliopo kwenye wimbo huo uliwaweka kwenye wakati mgumu Rachel Roy na Rita Ora ambao walidaiwa kuchepuka na bosi huyo wa lebo ya Roc Nation.
Skendo hiyo ilitia shaka kuvunjika kwa ndoa yao kutokana na yale aliyoyazungumza Queen Bey ndani ya albamu hiyo. Maisha yamezidi kuendelea huku wawili hao wakionekana kwenye viwanja mbalimbali wakiendelea kula bata pamoja huku ndoa yao ikizidi kuwa na furaha na Jay Z akizidi kutoa mchango mkubwa kwenye ziara ya Beyonce, ‘Formation Tour’.
Ukweli unaonesha kuwa Jay alikubali kuimbwa hivyo na mkewe kwa imani iliyotimia kuwa albamu ya Lemonade ingeingiza mkwanja mrefu na mwisho wa siku wawili hao wataendelea kufurahia mapenzi yao, na mahaba tele. Hiyo inathibitika kama alivyorap Jay Z kwenye mashairi ya remix ya Fat Joe na Remy Ma, “You know you made it when the fact your marriage made it is worth millions. Lemonade is a popular drink and it still is.”
Tazama picha za Queen Bey na Jay Z baada ya Lemonade kutoka na wakifurahia vekesheni ya nguvu