Cameron kuondoka madarakani Uingereza
Cameron kuondoka madarakani Uingereza Image copyright PA Image caption Bw Cameron na Bi Theresa May Leo ni siku ya mwisho kwa David Camer...
http://clemencekarani.blogspot.com/2016/07/cameron-kuondoka-madarakani-uingereza.html
Cameron kuondoka madarakani Uingereza
Leo ni siku ya mwisho kwa David Cameron kushikilia wadhifa wa waziri mkuu wa Uingereza baada ya kuhudumu kwa miaka 6.
Cameron alitangaza uamuzi wake kujiuzulu mwezi uliopita baada ya kushindwa katika kura ya maoni kuhusu uanachama katika Muungano wa Ulaya.
Anayemrithi ni Theresa May, aliyeidhinishwa kama kiongozi mpya wa chama cha Conservative Jumatatu.