Baada ya Thierry Henry kuambiwa achague moja na Arsene Wenger, hili ndio jibu lake….
Thierry Henry ameacha kazi kama kocha wa timu ya vijana ya Arsenal baada ya Arsene Wenger kumwambia achague moja, kubaki kuwa kocha na...
http://clemencekarani.blogspot.com/2016/07/baada-ya-thierry-henry-kuambiwa-achague.html
Thierry Henry ameacha kazi kama kocha wa timu ya vijana ya Arsenal baada yaArsene Wenger kumwambia achague moja, kubaki kuwa kocha na kuweka muda wake wote kwenye kazi hio au kuendelea kuwa mchambuzi wa mambo ya soka kwenye vituo vya tv kama Sky na BBC.
Wenger amempa nafasi Henry ya kuchagua kazi gani anataka kufanya na iwe moja tu na ndipo Henry alipomuambia kwaheri baba.
Wenger mwenye umri wa miaka 66 anasema Henry hawezi kuwa kocha wa Arsenalkwenye siku za wiki alafu wikiend anawaponda wachezaji wetu.
Henry aliyekuwa mshambuliaji mkubwa wa Arsenal ataendela na kazi za uchambuzi kwenye vituo vya tv kama BBC alivyofanya kwenye michuano ya Euro 2016 na Sky Sports ambapo analipwa Pound milioni 4 kwa mwaka